• Log In
    New user? Click here to register.Have you forgotten your password?
  • Communities & Collections
  • All of Repository
  • Log In
    New user? Click here to register.Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Mnenuka, Angelus"

Now showing 1 - 3 of 3
Results Per Page
Sort Options
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Mizimu katika Ngano za Kiafrika: Uchambuzi wa Ngano Teule
    (TUKI, 2020) Mnenuka, Angelus
    Fasihi simulizi ni sanaa inayotumia mbinu mbalimbali za kifani kujadili masuala anuwai katika jamii. Miongoni mwa mbinu za kifani zinazotumiwa kuyajadili masuala ya kijamii katika fasihi simulizi ni pamoja na matumizi ya wahusika wanaojulikana na watumiaji wa sanaa hiyo. Hii ina maana kwamba ili kufanikisha malengo yake, wahusika wanaosawiriwa katika fasihi simulizi mara nyingi wanajulikana kwa hadhira. Ingawa wahusika wengi wa fasihi simulizi hujulikana, baadhi hawaonekani katika jamii kwa kutumia milango mitano ya fahamu. Swali kuu ambalo linajadiliwa katika makala haya ni: Je, wahusika kama vile mizimu ambao hawaonekani kwa kutumia milango ya fahamu wanasawiriwaje katika fasihi simulizi? Katika makala haya tunachunguza usawiri wa mizimu katika ngano kwa kutumia Nadharia ya Ontolojia ya Kiafrika. Kimsingi, lengo kuu la makala haya ni kuonesha uhusiano uliopo baina ya mizimu katika ngano na Ontolojia ya Kiafrika. Kwa kuzingatia nduni bainifu za mizimu kama zilivyojadiliwa na wanazuoni mbalimbali, tumebaini kuwa mizimu, yaani wahenga na mazimwi ni dhana zilizochopolewa katika imani za Kiafrika, yaani ni sehemu ya Ontolojia ya Kifrika. Uhusiano baina ya mizimu yenyewe, na uhusiano baina ya mizimu na binadamu kimamlaka katika ngano unaweza kufafanuliwa vizuri kwa kutumia Nadharia ya Ontolojia ya Kiafrika. Kwa hiyo, ontolojia ya jamii ni msingi katika uhakiki wa kazi za fasihi, kwa sababu wahusika pamoja na usawiri wao huathiriwa kwa kiasi kikubwa na mtazamo wa jamii kuhusu wahusika na uhusiano baina ya wahusika.
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Public Policy Challenges in Tanzania as Portrayed in Swahili Written Literature
    (TUKI, 2019) Mnenuka, Angelus
    Tanzania has experienced significant policy changes in more than 50 years since independence. In the 1960s, after independence, Tanzania adopted Ujamaa, which aimed at uniting her citizens by eradicating exploitation among people. However, the policy eventually proved economically unsuccessful. Reasons for the downfall of Ujamaa include mismanagement of the public institutions and public funds embezzlements by state officials. This policy was followed by liberalisation policies which led the government to entrust public means of production to individuals. Like historical sources, the literary world has its own ways of discussing such matters. This paper seeks to discuss how such policies surface in Swahili written literature by expounding views for each policy.
  • No Thumbnail Available
    Item
    Utendajipepe wa Fasihi Simulizi: Haja ya Kuwa na Tawi Jipya
    (Taylor & Francis Group, 2019-11-24) Mnenuka, Angelus
    Makala hii inajadili dhana ya utendaji wa fasihi simulizi mtandaoni. Kiini cha makala hii ni hoja kuwa uainishaji wa fasihi hivi sasa, yaani fasihi simulizi na fasihi andishi, umekitwa katika aina za uwasilishaji, ambazo ni uwasilishaji wa kimazungumzo na wa kimaandishi. Ugunduzi wa intaneti, na kuingia kwa teknolojia hiyo katika vifaabebe kama vile simu na sleti2 kwa kutumia programu mbalimbali za kuwasiliana, umewezesha mawasiliano ya kimaandishi ya papo kwa papo au yasiyo ya papo kwa papo. Mawasiliano hayo yamechangia kuibuka kwa lugha ya kipekee ambayo sifa zake hazifanani na sifa ya lugha ya kimazungumzo wala lugha ya kimaandishi. Licha ya kuwa na lugha ya kipekee, baadhi ya tanzu za fasihi simulizi, kwa namna ya kipekee, zimekuwa zikitendeka mtandaoni kwa kutumia lugha hiyohiyo. Utafiti huu umefanyika kwa kutumia Nadharia ya Utendaji bila kuathiri nafasi na umuhimu wa matini katika kazi za kifasihi.3 Data za utendaji wa vitendawili mitandaoni zilikusanywa, zilichambuliwa, na matokeo yake yanawasilishwa katika makala hii. Kwa kutumia utendaji wa vitendawili vya Kiswahili mtandaoni, ninapendekeza liundwe tawi jipya la fasihi ambalo litafumbata sifa za aina hiyo ya mawasiliano.

University of Dar es Salaam © 2025

  • RIMS
  • UDSM MAIL
  • ARIS
  • LIBRARY REPOSITORY